Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Lengo & Majukumu ya OMPR

Lengo la OMPR : Lengo   la   kuanzishwa   Afisi   ya   Makamu   wa   Pili   wa   Rais   ni   kuratibu   na kusimamia  shughuli  zote  za  Serikali  ya  Mapinduzi  ya  Zanzibar  na  zile  za Serikali  ya  Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania  zinazohusiana  na  masuala ya Muungano.

Majukumu ya OMPR

a. Kutoa  huduma  kwa  Mheshimiwa  Makamu  wa  Pili  wa  Rais  katika  ofisi  na makaazi yake;

b. Kuratibu  shughuli   za  Serikali  ya  Mapinduzi  ya  Zanzibar   na  mambo  ya Muungano ambayo yanajumuisha:

  1. Kuhakikisha   kwamba   Taasisi   za   Serikali   ya   Mapinduzi   ya   Zanzibar zinatoa huduma bora kwa umma;
  2. Kusimamia    miradi    yote    ya    Serikali    ya    Jamhuri    ya    Muungano inayotekelezwa Zanzibar;
  3. Kusimamia   kazi   za   Taasisi   za   Serikali   ya   Jamhuri   ya   Muungano zinazofanya shughuli zake Zanzibar;
  4. Kuratibu   shughuli   za   kukabiliana   na   maafa   kwa   kuweka   mifumo imara   ya   kujikinga,   kujiandaa   na   kukabiliana   na   majanga   kabla, wakati na baada ya kutokea;
  5. Kuratibu  sherehe  na  maadhimisho  ya  kitaifa  pamoja  na  shughuli  za kuwaenzi viongozi wa  kitaifa kama ilivyoelekezwa katika Sheria Namba 5 ya 2019;

c. Kusimamia kazi za Baraza la Wawakilishi na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar.